MABINGWA watetezi, Yanga SC wamefanikiwa kwenda Raundi ya Tatu ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya ushindi wa 8-0 dhidi ya Kurugenzi ya leo Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Yanga leo yamefungwa na Clement Mzize manne dakika za kwanza, nane, 41 na 45 na ushei, Jefta John aliyejifunga dakika ya sita, David Bryson dakika ya 77 na Yussuf Athumani mawili dakika ya 79 na 85.
0 comments:
Post a Comment