Mabao ya Coastal Union yamefungwa na kiungo Mrundi, Emery Nimubona dakika ya 29 na mshambuliaji Mcameroon, Vincent Abubakar dakika ya 49, wakati la Singida Big Stars limefungwa na Deus Kaseke kwa penalti dakika ya 90 na ushei.
Kwa ushindi huo, Coastal Union inakamilisha mechi 15 za mzunguko wa kwanza ikiwa na pointi 15 na kupanda kwa nafasi moja hadi ya 12, wakati Big Stars inabaki na pointi zake 27 za mechi 15 pia nafasi ya nne.
0 comments:
Post a Comment