TIMU ya Taifa ya Morocco imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Dunia baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Ureno leo Uwanja wa Al Thumama Jijini Doha.
Bao pekee la Simba wa Atlasi katika mchezo huo limefungwa na Youssef En-Nesyri dakika ya 42 na sasa Morocco ambayo inakuwa nchi ya kwanza ya Afrika kufika Nusu Fainali ya Kombe la Dunia itakutana na Ufaransa iliyoitoa England kwa kuichapa 2-1.
0 comments:
Post a Comment