• HABARI MPYA

    Tuesday, December 06, 2022

    KOMBE LA DUNIA QATAR 2022 NA MGUSO WA KIPEKEE KWA WATANZANIA

    MWANZONI mwa mwaka huu unaoelekea ukingoni, Wakati ikielezwa namna Kombe la FIFA la Dunia kwa mwaka huu wa 2022 litakuwa na msisimko wa kipekee,wengi walikuwa na maswali kadhaa yaliyohitaji majibu.
    Ikiwa zimetimia takribani wiki 2 na siku kadhaa tangu michuano hii kuanza kutimu vumbi huko nchini Qatar maswali haya kutoka kwa mashabiki wengi wa soka yanathibitika kujibiwa na kiu inakatwa.
    Ubunifu wa kimandhari…teknolojia ya kushangaza, matokeo ya kustaajabisha ikiwemo Taifa la Japan kuwachalaza vigogo wa soka kutoka barani ulaya, Ujerumani na Hispania. 
    Bila kusahau mataifa ya Ubelgiji na Ujerumani kuaga mashindano katika hatua ya makundi...Yote haya yameongeza nafasi na ladha ya kipekee kunako Kombe la Dunia mwaka huu. 


    Habari njema zaidi kwa watanzania mwaka huu ni ukweli na uhakika kwamba shindano hili kubwa zaidi kisoka ulimwenguni limekuwa likiruka LIVE na kwa muonekano wa HD kupitia chaneli ya taifa TBC kupitia vyombo vyake bora vya Tbc1, Tbc Taifa, Tbc Fm na Tbc Online. 
    Inafurahisha sana kusikia sauti za furaha na vifijo kwa watanzania katika vyombo vya usafiri,maeneo ya biashara,makazi na hata taasisi za kitaaluma juu ya shindano hili huku wote wakitumia chombo cha Taifa TBC, kuwaunganisha na matukio ya kile kinachojiri nchini Qatar bure kabisa (FTA).
    Watazamaji wa soka Tanzania wana mengi ya kufurahia juu ya hili, shukrani kwa TBC kwa kupata haki za kuonyesha mashindano haya bure (FTA), mijini na vijijini hivi sasa kuna furaha juu ya Kombe la Dunia Qatar-2022.
    Chaneli hii ya Taifa inapatikana bure kwenye visimbuzi vya aina zote, yaani vya malipo na vile vya bure hapa nchini.
    Kwa kutumia Startimes Tanzania na Azam Tv ambao wanaruhusa kisheria kusambaza matangazo ya TBC bure kote Tanzania, Shirika hili la Taifa limekata kiu na linaendelea kutimiza ahadi yake ya kuwapatia burudani ya takribani michezo 28 ya michuano hii kupitia TBC1 huku michezo yote 64 ya mashindano ikiwafikia watanzania kupitia TBC Taifa na TBC Fm (matangazo ya redio).
    TBC1 inapatikana katika chaneli namba 101 katika Antenna na chaneli namba 445 kupitia Dishi ndani ya kisimbuzi cha Startimes, kisimbuzi chenye watumiaji wengi zaidi nchini.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KOMBE LA DUNIA QATAR 2022 NA MGUSO WA KIPEKEE KWA WATANZANIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top