WENYEJI, Chelsea jana wameibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya West Ham United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Stamford Bridge, London.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na Ben Chilwell dakika ya 76 na Kai Havertz dakika ya 88 baada ya Michail Antonio kuitanguliza West Ham kwa bao lake la dakika ya 62.
West Ham United walidhani wamesawazisha baadaye, lakini bao la Maxwel Cornet lilikataliwa baada ya msaada wa VAR.
0 comments:
Post a Comment