MABAO ya Jack Grealish dakika ya kwanza, Erling Haaland dakika ya 16 na Phil Foden dakika ya 69 leo yameipa Manchester City ushindi wa 3-0 dhidi ya wenyeji, Wolverhampton Wanderers katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Molineux.
Man City inafikisha pointi 17 katika mchezo wa saba na kuendelea kuongoza ligi hiyo kwa wastani tu wa mabao dhidi ya Tottenham Hotspur baada ya wote kucheza mechi saba.
Tottenham leo imeitandika Leicester City 6-2 Uwanja wa Tottenham Jijini London.
0 comments:
Post a Comment