BAO pekee la Simon Happygod Msuva dakika ya 28 limeipa Tanzania ushindi wa 1-0 dhidi ya Uganda katika mchezo wa kirafiki wa Kimataifa usiku wa Ijumaa Uwanja wa Modern Jijini Benghazi, Libya.
Taifa Stars itashuka tena dimbani Jumanne kumenyana na wenyeji, Libya katika mchezo wa mwisho wa kirafiki ulio katika kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), kabla ya kurejea nyumbani.
0 comments:
Post a Comment