BONDIA Twaha Kassim Rubaha juzi usiku alimshinda Abdo Khalid wa Misri Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara na kutetea ubingwa wa UBO Afrika huku akiongeza taji la Mabara la UBO.
Kulikuwa kuna mapambano mengine kadhaa ya utangulizi, likiwemo la bondia 'kichekesho' Karim Mandonga wa Morogoro ambaye kama kawaida lichapwa kwa Knockout (KO) na Salim Abeid wa Tanga. Naye Adam Lazaro alimshinda kwa pointi mkongwe Francis Miyeyusho katika pambano lingine tamu la utangulizi usiku huo. Mtoto wa nyumbani, Mtwara Osama Arabi 'akafundishwa' ndondi na mkongwe wa Emmilian Patrick wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika pambano lililovutia wengi. Joseph Mchapeni akamchapa Paschal Goba kwa pointi katika pambano lingine lililoteka hisia za wengi usiku huo Uwanja wa Nangwanda Sijaona.
'The abuse was too much to handle': Chelsea defender Millie Bright reveals
reasons for her shock retirement
-
Bright - who won the Euros with England in 2022 and reached the World Cup
final a year later - provided more clarity on her decision, and opened up
on the ...
1 hour ago


.png)
0 comments:
Post a Comment