BONDIA Twaha Kassim Rubaha juzi usiku alimshinda Abdo Khalid wa Misri Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara na kutetea ubingwa wa UBO Afrika huku akiongeza taji la Mabara la UBO.
Kulikuwa kuna mapambano mengine kadhaa ya utangulizi, likiwemo la bondia 'kichekesho' Karim Mandonga wa Morogoro ambaye kama kawaida lichapwa kwa Knockout (KO) na Salim Abeid wa Tanga. Naye Adam Lazaro alimshinda kwa pointi mkongwe Francis Miyeyusho katika pambano lingine tamu la utangulizi usiku huo. Mtoto wa nyumbani, Mtwara Osama Arabi 'akafundishwa' ndondi na mkongwe wa Emmilian Patrick wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika pambano lililovutia wengi. Joseph Mchapeni akamchapa Paschal Goba kwa pointi katika pambano lingine lililoteka hisia za wengi usiku huo Uwanja wa Nangwanda Sijaona.
Arsenal vs Chelsea - Premier League: Live score, team news and updates as
Mikel Arteta's side can stretch their lead at the top of the Premier League
to three points with a win
-
Follow Mail Sport's live blog for the latest score, team news and updates
as Arsenal host Chelsea in Premier League action.
7 minutes ago
0 comments:
Post a Comment