TIMU ya Geita Gold imechapwa 1-0 na wenyeji, Al Hilal Port Sudan katika mchezo wa kwanza Raundi ya Awali Kombe la Shirikisho Afrika usiku huu Uwanja wa Al-Hilal mjini Omdurman.
Bao pekee la Al Hilal limefungwa na Omer Shamali dakika ya tano na timu hizo zitarudiana Septemba 17 Uwanja Azam Complex, Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na mshindi wa jumla atamenyana na Pyramids ya Misri katika Raundi ya Pili.
0 comments:
Post a Comment