TANZANIA imevuliwa ubingwa wa COSAFA Wanawake baada ya kuchapwa 2-1 na Zambia leo Uwanja wa Isaac Wolfson mjini Port Elizabeth, Afrika Kusini.
Mabao ya Zambia yamefungwa na Barbara Banda dakika ya 11 na Chisha Misozi dakika ya 46, wakati la Twiga Stars alijifunga Margaret Balemu dakika ya 30. Twiga Stars sasa itawania nafasi ya tatu.
0 comments:
Post a Comment