BAO pekee la Jeremiah Juma dakika ya 46, limeipa Tanzania Prisons ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Kwa ushindi huo, Tanzania Prisons wanafikisha pointi saba na kusogea nafasi ya nane, wakati Azam FC inabaki na pointi zake nane ikishukia nafasi ya sita baada ya wote kucheza mechi tano.
0 comments:
Post a Comment