MABAO ya Fede Valverde dakika ya 80 na Marco Asensio dakika ya 90 na ushei yameipa Real Madrid ushindi wa 2-0 dhidi ya RB Leipzig katika mchezo wa Kundi F Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa Jumatano Uwanja wa Santiago Bernabéu Jijini Madrid.
Real Madrid inafikisha pointi sita na kuendelea kuongoza Kundi F mbele ya Shakhtar Donetsk yenye pointi nne na Celtic pointi moja, wakati RB Leipzig inashika mkia ikiwa haina pointi baada ya wote kucheza mechi mbili.
0 comments:
Post a Comment