MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla leo ametembelea uwanja wa klabu ya Simba, Mo Simba Arena uliopo Bunju na kuwapa siku 60 waliovamia eneo hilo kuhama.
Pamoja na hayo, Makalla ameiruhusu Simba SC kuendelea na mradi wa ujenzi wa ukuta kuzunguka eneo la Uwanja huo.
Na Mkandarasi aliyepewa tenda ya ujenzi huo alifika pia kwenye eneo hilo kufanya tathmini ya mwisho tayari kuanza kazi.
0 comments:
Post a Comment