• HABARI MPYA

    Tuesday, September 20, 2022

    KMC YAICHAPA IHEFU SC 2-1 UWANJA WA UHURU


    WENYEJI, KMC wameibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Ihefu SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
    Mabao ya KMC yamefungwa na Matheo Anthony dakika ya tatu na Nzigamasabo Steve dakika ya 77, wakati la Ihefu SC limefungwa na Raphael Daudi dakika y 34.
    KMC inafikisha pointi tano baada ya ushindi huo ikisogea nafasi ya nane, wakati Ihefu inaendelea kuwa timu pekee ambayo haijavuna pointi hadi sasa kufuatia wote kucheza mechi nne.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KMC YAICHAPA IHEFU SC 2-1 UWANJA WA UHURU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top