KLABU ya Azam FC imemsajili winga wa kimataifa wa Zambia, Charles Zulu, kwa mkataba wa miaka miwili kutoka Cape Town City ya Afrika Kusini.
Taarifa ya Azam FC leo imesema kwamba
wamemsajili Zulu baada ya kufikia makubaliano na Cape Town City, aliyokuwa akiichezea.
Zulu ambaye wakala wake ni Nir Karin, ataanza kuitumikia Azam FC msimu ujao 2021/22, ambapo kabla ya kutua Afrika Kusini alikuwa akikipiga kwa vigogo wa Zambia, Zanaco FC.
Na amesaini mkataba huo baada ya kufuzu vipimo vya Afya.
0 comments:
Post a Comment