Edin Visca (kulia) akimtungua kipa wa Manchester United, Dean Henderson kuwapatia wenyeji, Istanbul Basaksehir bao la pili dakika ya 40 kufuatia Demba Ba kufunga la kwanza dakika ya 12 katika ushindi wa 2-1 kwenye mchezo wa Kundi H Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana Uwanja wa Basaksehir Fatih Terim Jijini İstanbul. Pamoja na kipigo hicho, Man United ambayo bao lake lilifungwa na Anthony Martial dakika ya 43 wanaendelea kuongoza kundi kwa pointi zao sita, sawa na RB Leipzig wote wakifuatiwa na PSG na Istanbul Basaksehir zenye pointi tatu kila moja baada ya timu zote kucheza mechi tatu PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment