• HABARI MPYA

    Wednesday, January 25, 2017

    SIMBA KWA HILI LA LUFUNGA HAWACHOMOKI

    Na Yossima Sitta Jr., DAR ES SALAAM
    KWA sasa mitandao ya kijamii iko busy kuulizia kanuni na uhalali wa Novart Lufunga kuwepo kwenye mchezo wa Jumamosi  dhidi ya Polisi Dar kwenye kombe la Azam Sports federation Cup. Mchezo ulimalizika kwa Simba Sc kushida kwa magoli mawili kwa bila na kufanikiwa kutinga  hatua ya Sita (16 bora ) 
    -Baada ya kuona  mitandao iko busy na mimi nikaona niingie chimbo kidogo kufatilia na kuangalia kanuni na data zinasemaje kuhusu uwepo wa Novart Lufunga kwenye dhidi ya Polisi Dar . 

    Novaty Lufunga (kushoto) anadaiwa kuhusika katika mechi ya Kombe la TFF akiwa anatumikia adhabu ya kadi

    Kanuni 
    a) Mchezaji ambaye unakuwa na kadi tatu za njao atakosa mchezo mmoja unaofuata
    b)Mchezaji ambaye amepata kadi nyekundu ya mojaa kwa mojaa atakosa michezo miwili inayofuata
    c)Mchezaji ambaye amepati kadi ya pili ya njano na kuwa nyekundu ndani ya mechi mojaa  atakosa mechi mojaa inayofuata . 

    Data 
    a)Novart Lufunga alicheza mechi ya April 11 dhidi ya Coastal Union kwenye ASFC mechi ya hatua ya robo fainali mchezo uliofanyika uwanja wa Taifa na na Coastal Union kushida GOLI mojaa kwa bila na  kutinga hatua ya nusu Fainal 
    b)Novart Lufunga Alimchezea madhambi Ally Shiboli wa Coastal ndani ya 18 na kusababisha penati ambapo mwamuzi wa mchezo huo alimpa kadi ya pili ya njano na kuwa nyekundu 
    c)Novart Lufunga alikuwepo kwenye kikosi cha Simba  April 17 cha ligi Kuu VPL dhidi ya Mwadui FC (kikosi check picha )
    d)Novart Lufunga alikuwepo kwenye wachezaji wa akiba mechi ya Jumamosi dhidi ya Polisi dar kwenye mchezo wa ASFC Ukiwa mchezo uliofuata wa ASFC baada wa ule dhidi ya Coastal Union (kikosi check picha ) 

    Sheria za TFF 
    -Sheria za Soka za TFF zinasema kama timu ikimchezesha mchezaji Mwenye kadi tatu za njano au nyekundu itanyang'anywa ushidi na kupewa timu waliocheza nayo pamoja na magoli matatu. 
    Mfano . Timu ya Azam FC ilinyang'anywa ushidi na point tatu na kupewa ya Mbeya city baada ya kujiridhisha walimchezesha akiwa na kadi tatu za njano.

    Swali la kujiuliza 
    ? Je  TFF wanasemeje kuhusu kuunganisha michuano hii ya ASFC na Ligi Kuu ? 
    Yaani Mchezaji alipata kadi nyekundu kwenye ligi Kuu anaweza akaitumia kwenye kombe la ASFC kama wanavyofanya Uingereza maana makombe yote yanajumuishwa ulipata kadi kwenye kombe la Capital one unaweza ukaitumia kwenye ligi Kuu au FA cup . 
    TFF WANARUHUSU HII? 

    majibu 
    1-Kama Ndio 
    Simba Sc inatakiwa kukatwa Ilitakiwa kukatwa point kwenye ligi Kuu iliyomalizika na kupewa timu ya Mwadui FC na magoli matatu 
    (Ingawa mechi hii Mwadui walishida  kwa GOLI mojaa kwa bila )
    2-Kama Hapana 
    Simba wanatakiwa kunyang'anywe ushidi wao wa Jumamosi na kupewa Polisi Dar na kuendelea na hatua ya 16 bora .

    Maswali mengine ya kujiuliza 
    1-Je polisi Dar imekata rufaa kuhusu kuchezeshwa kwa Lufunga? He sheria zinasemaje Mkataba rufaa inatakiwa kupata rufaa ndani ya masaa mangap?
    2-Je Kama kanuni zitataka Simba Sc kukatwa pointi watakatwa za msimu ulioisha au msimu huu? 
    3-Je Maneja Wa Simba Ally Abbas wakati unamkabidhi mafaili ya umeneja Mgossi hukumkabidhi Faili  la Lufunga? 

    Ally Abbas au Mussa Mgossi
    -Kama kweli uzembe huu atabebeshwa mmoja kati ya Abass au mgosii kwa uzembe kama Mgossi alipewa mafaili lazima atakuwa anajua na alipaswa amkumbushe kocha aache kumtumia Lufunga hata hivyoo mechi hyoo Mgossi alikuwa bechi 
    (Mwandishi wa makala haya, Yossima Sitta Jr., ameitambulisha kama msomaji wa tovuti hii namba moja ya Kiswahili ya michezo duniani)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA KWA HILI LA LUFUNGA HAWACHOMOKI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top