Mshambuliaji wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic akipiga mpira kichwa mbele ya beki wa Hull City, Michael Dawson usiku wa jana katika mchezo wa marudiano Nusu Fainali Kombe la Ligi England usiku wa jana Uwanja wa KCOM. Hull City walishinda 2-1, lakini wametolewa kwa jumla ya mabao 3-2, baada ya kufungwa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza na United sasa itakutana na Southampton katika fainali Februari 26 Uwanja wa Wembley. Mabao ya Hull jana yalifungwa na Tom Huddlestone kwa penalti dakika ya 35 na Oumar Niasse dakika ya 85, wakati la United lilifungwa na Paul Pogba dakika ya 66 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Watch: Lille midfielder Ethan Mbappe shown red card for ugly elbow
-
Ethan Mbappé was shown a red card in Lille's Champions League match against
Real Betis on Tuesday.
13 hours ago



.png)
0 comments:
Post a Comment