• HABARI MPYA

    Sunday, November 15, 2015

    TAIFA STARS NA ALGERIA ZILIVYOTOANA JASHO JANA UWANJA TAIFA

    Mshambuliaji wa Tanzania, Mrisho Ngassa akimtoka beki wa Algeria, Mesloub Wald katika mchezo wa kwanza Raundi ya Pili kufuzu Kombe la Dunia 2018 jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka sare ya 1-1 na zitarudiana Jumanne - na mshindi wa jumla atafuzu hatua ya mwisho ya mchujo, ambayo itakuwa ya makundi.

    Mshambuliaji wa Tanzania, Mbwana Samatta akimtoka kipa wa Algeria, M'bolhi Rais (kulia) baada ya kumlamba chenga lakini akapiga nje ya lango. Kushoto ni Ghoulam Faouzi wa Algeria

    Benchi la Ufundi la Tanzania, kutoka kushoto Kocha Mkuu, Charles Boniface Mkwasa, Kocha Msaidizi Hemed Morocco na Mshauri wa Ufundi, Alhaj Abdallah Athumani Seif 'King Kibadeni' wakifuatilia mchezo

    Mshambuliaji wa Tanzania, Thomas Ulimwengu (kushoto) akitafuta maarifa ya kumtoka beki wa Algeria

    Winga wa Tanzania, Farid Mussa (kulia) akiwania mpira dhidi ya beki wa Algeria, Zeffanne Mehdi

    T
    Kiungo wa Tanzania, Mudathir Yahya (kushoto) akimlamba chenga beki wa Algeria (Taider Saaphir)

    Beki wa Tanzania, Shomary Kapombe akitafuta maarifa ya kumpita beki wa Algeria, Medjan Carl

    Mshambuliaji wa Tanzania, Elias Maguri (kushoto) akitafuta maarifa ya kumpokonya mpira beki wa Algeria, Mandi Issa

    Kikosi cha Taifa Stars jana

    Kikosi cha Algeria jana

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS NA ALGERIA ZILIVYOTOANA JASHO JANA UWANJA TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top