• HABARI MPYA

    Friday, November 27, 2015

    KING KIBADEN: TUTACHEZA KWA TAHADHARI KUHIFADHI NGUVU KWA AJILI YA ROBO FAINALI

    RATIBA KOMBE LA CHALLENGE 2015
    Leo; Novemba 27, 2015
    Rwanda Vs Somalia
    Zanzibar Vs Kenya
    S. Sudan v Malawi
    Djibouti V Sudan
    Kesho; Novemba 27, 2015
    Uganda Vs Burundi 
    Tanzania Vs Ethiopia
    King Kibaden amesema leo watacheza kwa tahadhari nguvu zao kwa ajili ya Robo Fainali 

    Na Mwandishi Wetu, ADDIS ABABA
    KOCHA Mkuu wa Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’ amesema kwamba leo watacheza kwa tahadhari ili kutunza nguvu zao kwa ajili ya Robo Fainali.
    Kili Stars inamenyana na wenyeji, Ethiopia kesho katika mchezo wa mwisho wa Kundi A michuao ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge mjini Addis Ababa, Ethiopia.
    Na Kibadeni amesema watapigania ushindi, lakini hawatatumia nguvu nyingi kukwepa kujichosha na wachezaji kuumia, wakati timu imekwishatinga Robo Fainali.
    “Tunajua wenzetu wanataka sana ushindi ili waende Robo Fainali. Na kwa sababu ni wenyeji, tunatarajia hata marefa watakuwa upande wao. Tutajaribu kupambana tusipoteze mchezo. Hilo ndilo kubwa,”amesema Kibadeni.
    Kwa ujumla mshambuliaji huyo wa zamani wa kimataifa nchini, amesema wachezaji wake wako vizuri kuelekea mchezo wa jioni ya leo na ana matumaini ya ushindi.
    Kili Stars imejihakikishia Robo Fainali baada ya ushindi mfululizo katika mechi mbili za awali, 4-0 dhidi ya Somalia na 2-1 dhidi ya Rwanda na leo inakamilisha mechi zake za Kundi A ikiwa kileleni. 
    Mechi za makundi za Challenge 2015 zinahitimishwa leo Rwanda ikimenyana na Somalia, Zanzibar na Kenya, Sudan Kusini na Malawi, Djibouti na Sudan, wakati kesho Uganda itamenyana na Burundi na Tanzania na Ethiopia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KING KIBADEN: TUTACHEZA KWA TAHADHARI KUHIFADHI NGUVU KWA AJILI YA ROBO FAINALI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top