• HABARI MPYA

    Friday, November 27, 2015

    LIVERPOOL YAENDELEA KUNG’ARA ULAYA, SPURS NAYO YATOA ADHABU UGENINI

    MATOKEO MECHI ZA UEFA EUROPA LEAGUE JANA
    Novemba 26, 2015  
    PAOK Salonika 0-0 FK Qabala
    Club Brugge 0-1 Napoli
    Sporting Braga 2-1 Slovan Liberec
    Molde 0-2 Fenerbahce
    Marseille 2-1 FC Groningen
    Liverpool 2-1 Bordeaux
    Villarreal 1-0 SK Rapid Wien
    Celtic 1-2 Ajax
    Legia Warsaw 1-0 FC Midtjylland
    FK Qarabag 0-1 Tottenham Hotspur
    FC Augsburg 2-3 Athletic Club
    Sparta Prague 1-0 Asteras Tripolis
    FC Basel 2-2 Fiorentina
    FC Schalke 04 1-0 APOEL Nicosia
    Monaco 0-2 RSC Anderlecht
    AZ 1-2 Partizan Belgrade
    Lazio 3-1 Dnipro Dnipropetrovsk
    Lokomotiv Moscow 2-4 Sporting Lisbon
    Rosenborg 1-1 St Etienne
    Belenenses 0-0 Lech Poznan
    Besiktas 2-0 Skenderbeu Korce
    FK Krasnodar 1-0 Borussia Dortmund
    Rubin Kazan 2-0 FC Sion
    Dinamo Minsk 1-0 Viktoria Plzen

    Wachezaji wa Liverpool wakimpongeza Benteke baada ya kufunga jana PICHA ZAIDI GONGA HAPA

    BAO pekee la Harry Kane dakika ya 78 limeipa Tottenham Hotspur ushindi wa 1-0 dhidi ya FK Qarabag ugenini katika mchezo wa Europa League Uwanja wa Tofik Bakhramov jana.
    Kwa ushindi huo, Spurs inapanda kileleni mwa Kundi J baada ya kufikisha pointi 10 kutokana na mechi tano ilizochea. Mchezo mwingine wa kundi hilo, RSC Anderlecht imeshinda ugenini pia 2-0 dhidi ya Uwanja wa Louis II, mabao ya Guillaume Gillet dakika ya 46 na Frank Acheampong dakika ya 78.
    Liverpool imepanda kileleni mwa Kundi B baada ya kushinda mabao 2-1 dhidi ya Bordeaux jana Uwanja wa Anfiled na kufikisha pointi tisa za mechi tano. 

    Harry Kane akikimbia kushangilia baada ya kuifungia Tottenham katika Europa League jana PICHA ZAIDI GONGA HAPA

    Mabao ya Liverpool yamefungwa na James Milner kwa penalti dakika ya 38 na Christian Benteke dakika ya 46, wakati la wageni limefungwa na Henri Saivet dakika ya 33.
    Mchezo mwingine wa kundi hilo, Rubin Kazan imeshinda 2-0 dhidi ya FC Sion mabao ya Blagoy Georgiev dakika ya 72 na Marko Devic dakika ya 90 Uwanja wa Kazan Arena.
    Matokeo hayo, yanazifanya zote, Liverpool na Spurs zijihakikishie kutinga hatua ya mtoano ya michuano hiyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL YAENDELEA KUNG’ARA ULAYA, SPURS NAYO YATOA ADHABU UGENINI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top