• HABARI MPYA

    Monday, November 23, 2015

    MALAWI YAIPIGA SUDAN 2-1, SUDAN KUSINI YAWALAZA 2-0 DJIBOUTI

    MATOKEO NA RATIBA CHALLENGE 2015
    Novemba 21, 2015
    Burundi 1-0 Zanzibar 
    Ethiopia 0-1 Rwanda
    Novemba 22, 2015
    Somalia 4-0 Tanzania 
    Kenya 2-0 Uganda 
    Novemba 23, 2015
    Sudan Kusini 2-0 Djbouti 
    Sudan 1-2 Malawi
    Kesho; Novemba 24, 2015
    Zanzibar Vs Uganda 
    Rwanda Vs Tanzania 
    Malawi imeanza vyema michuano ya Challenge 2015

    WAALIKWA, Malawi ‘Flames’ wameanza vyema michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge baada ya kushinda mabao 2-1 dhidi ya Sudan katika mchezo wa Kundi C jioni ya leo nchini Ethiopia.
    The Flames walipata bao la kwanza dakika ya 15 kupitia kwa Chiukepo Msowoya, kabla ya Sudan  kusawazisha dakika tano baadaye kupitia kwa gwiji wake, Atahir El-Tahir.
    Dalitso Sailesi akaifungia Malawi bao la ushindi dakika ya 32 na tangu hapo walisota kusawazisha bila mafanikio, ikiwemo mkwaju wa penalti wa El-Tahir kuokolewa na kipa wa Malawi, Simplex Nthala.
    Katika mchezo uliotangulia, Sudan Kusini imeshinda 2-0 dhidi ya Djibouti mabao ya Bruno Martinez dakika ya 28 na Dominic Abuyo dakika ya 72.
    Ushindi huo unaifanya Sudan Kusini iongoze Kundi C kwa sasa. Malawi itamenyana na Djibouti katika mchezo ujao, wakati Sudan itacheza na Sudan Kusini.
    Michuano hiyo, inaendelea kesho kwa mchezo kati ya Zanzibar na Uganda Kundi B na Rwanda dhidi ya Tanzania Bara, Kundi A.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MALAWI YAIPIGA SUDAN 2-1, SUDAN KUSINI YAWALAZA 2-0 DJIBOUTI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top