• HABARI MPYA

    Thursday, October 01, 2015

    MBEYA CITY WABANWA NA TOTO, SARE 1-1 KIRUMBA

    TIMU ya Mbeya City imelazimisha sare ya kufungana bao 1-1 Toto Africans Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza katika mchezo wa kuhitimisha mzunguko wa tano wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
    Matokeo hayo yanaifanya Mbeya ifikishe pointi nne baada ya mechi tano, ikishinda moja, kufungwa tatu na kutoa sare moja, wakati Toto inafikisha pointi sita, baadaya sare tatu, ushindi mmoja na kufungwa moja.
    Mbeya City imelazimishwa sare ya 1-1 na Toto Africans mjini Mwanza

    Mbeya City inayofundishwa na Juma Mwambusi, ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata dakika ya 12 kupitia kwa Jacob Mahundi, kabla ya mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Edward Christopher kuisawazishia Toto ya kocha John Tegete dakika ya 74.
    Katika mechi za jana, mabingwa watetezi, Yanga SC waliendelea kung’ang’ania usukani wa Ligi Kuu kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji Mtibwa Sugar, Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
    Majimaji FC ilitoka sare ya 1-1 na Ndanda FC Uwanja wa Majimaji, Songea, Prisons ilitoka 0-0 na Mwadui FC Uwanja wa Sokoine, Mbeya na Simba SC imeshinda 1-0 dhidi ya Stand United Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MBEYA CITY WABANWA NA TOTO, SARE 1-1 KIRUMBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top