• HABARI MPYA

    Sunday, April 05, 2015

    SERAFIM TODOROV; BONDIA ALIYEMPIGA MAYWEATHER ULINGONI OLIMPIKI 1996, SASA AMEFULIA ILE MBAYA

    BONDIA mstaafu, Serafim Todorov, mtu wa mwisho kumshinda ulingoni Floyd Mayweather, sasa anaishi kwa mshahara wa dola za Kimarekani 370 kwa mwezi kutoka Serikali ya Bulgaria.
    Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 45, alimpiga Mayweather katika pambano la uzito wa Feather Nusu Fainali ya michuano ya Olimpiki mwaka 1996 mjini Atlanta, lakini leo maisha yake ni ‘mabovu’. 
    Nusu fainali hiyo iliisha kwa utata kutokana na refa kumuinua mkono juu kimakosa Mayweather, lakini Todorov ndiye aliyeshinda kwa pointi.
    Serafim Todorov is the last man to beat Floyd Mayweather, doing so at the 1996 Olympic Games in Atlanta
    Serafim Todorov ndiye bondia wa mwisho kumpiga Floyd Mayweather katika michezo ya Olimpiki mwaka 1996 mjini Atlanta
    Todorov lives in a remote town in Bulgaria
    Mayweather is one of the richest athletes in the world
    Todorov (kushoto) anaishi katika 'kichovu' Bulgaria wakati Mayweather ni mmoja wa wanamichezo tajiri duniani

    Todorov alipigwa na bondia wa Thailand, Somluck Kamsing katika Fainali ya Olimpiki mjini Atlanta 1996 na baada ya hapo akapigana mapambano sita tu ya ngumi za kulipwa, akishinda matano kati ya mwaka 1998 na 2003, kabla ya kupoteza moja mbele ya Toni Naskovski mjini Macedonia mwaka 1999.
    Mmarekani Mayweather anajiandaa kwa moja ya mapambano ya kihistoria katika ulimwengu wa ndondi dhidi ya Mfilipino Manny Pacquiao litakalofanyika mjini Las Vegas, Mei 2 na amekwishapigana mapambano 47 katika ngumi za kulipwa bila kupoteza hata moja.
    Kwa sasa Mayweather ni mwanamichezo tajiri zaidi duniani, wakati huo huo Todorov, anaishi katika nyumba moja ndogo mjini Pazardzhik, kusini mwa Bulgaria akichangia gari aina ya Volkswagen Polo na mkewe.
    The unbeaten American is regularly seen on social media showing off his piles of cash and jewellery
    Mayweather kwa sasa ni mwanamichezo tajiri duniani na amekuwa akiposti picha za utajiri wake kwenye mitandao ya kijamii

    “Naishi kwa msaada kidogo kutoka serikalini, lakini fedha ninazopata kutoka serikalini hazitoshi, familia yangu haina kazi. Ni vigumu hapa kwa sababu ni mji mdogo na kuna nafasi chache za kazi,”.
    “Napata kama Euros 500 kwa mwezi, lakini nalazimika kulipa madeni benki au mikopo, namiliki nyumba ndogo (apartment) nayoishi, lakini hapa bado kuna bili za kulipa,” amesema.
    “Nilikuwa nina nyumba kubwa nyumbani kwetu Peshtera, kilomita 20 kutoka hapa ninapoishi kwa sasa, lakini ilibidi niiuze kwa sababu sikuwa na fedha za kujikimu,” amesema.
    Todorov (right) is beaten by Somluck Kamsing in the featherweight final at the 1996 Atlanta Olympic Games
    Todorov (kulia) alipigwa na Somluck Kamsing katika fainali uzito wa Feather michezo ya Olimpiki mwaka 1996 mjini Atlanta
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SERAFIM TODOROV; BONDIA ALIYEMPIGA MAYWEATHER ULINGONI OLIMPIKI 1996, SASA AMEFULIA ILE MBAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top