• HABARI MPYA

    Thursday, January 02, 2014

    SIMBA SC ILIVYOWAPA ZAWADI NONO YA MWAKA MASHABIKI WAKE UWANJA WA AMAAN, MTOTO MESSI NI MOTO WA KUOTEA MITA ELFU

    Kiungo wa Simba SC, Ramadhani Singano 'Messi' akimlamba chenga ya hatari beki wa AFC Leopard ya Kenya, Joseph Shikokoti kabla ya kutia krosi iliyozaa bao pekee la Simba SC lililofungwa na Amri Kiemba jana Uwanja wa Amaan, Zanzibar katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mapinduzi. Simba ilishinda 1-0.
    Kiungo wa Simba SC, Ramadhani Chombo 'Redondo' akimtoka beki wa AFC Leopard
    Mabehewa, safari Kigoma mwisho wa Reli; Ramadhani Singano akiwatoka mabeki wa AFC Leopard, wa nyuma yake ni Mussa Mudde aliyewahi kuchezea Simba SC pia
    Kiungo wa Simba SC, Uhuru Suleiman akigombea mpira na beki wa AFC Leopard
    Mshambuliaji wa Simba SC, Amisi Tambwe akimiliki mpira mbele ya Joseph Shikokoti wa AFC Leopard
    Beki wa Simba SC akijiandaa kupiga krosi pembeni ya kiungo wa AFC Leopard, Oscar Kadenge kulia
    Kocha wa timu ya taifa ya Italia, Cesare Prandile akiwa ameshika mpira kabla ya kuudunda kuashiria ufunguzi wa michuano ya Kombe la Mapinduzi mwaka huu
    Kiungo wa Simba SC, Haroun Chanongo akimtoka beki wa AFC Leopard, Mussa Mudde
    Kipa wa AFC Leopard, Martin Masalia akiwa amedaka mpira mbele ya mshambuliaji wa Simba SC, Amisi Tambwe
    Mussa Mudde kaanguka kushoto, Issa Rashid 'Baba Ubaya' wa Simba SC kulia na mchezaji mwenzake, Chombo Redondo anajiandaa kwenda kuchukua mpira bila upinzani
    Kikosi cha Simba SC kilichowapa zawadi nzuri ya mwaka mpya mashabiki wake
    Kikosi cha AFC  Leopard
    Prandile akisalimiana na Haroun Chanongo
    Prandile akisalimiana na Awadh Juma, huku Singano naye akijiandaa kutoa mkono wake
    Mpenzi maarufu wa Simba SC, Charles Hamkah alikuwepo pamoja na mkewe jukwaani
    Simba SC 'Chama Kubwa'; Mashabiki Wazungu waliokuja kuishangilia Simba SC

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC ILIVYOWAPA ZAWADI NONO YA MWAKA MASHABIKI WAKE UWANJA WA AMAAN, MTOTO MESSI NI MOTO WA KUOTEA MITA ELFU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top