Na Mahmoud Zubeiry, Mombasa
MUSSA Katabaro, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu ya Yanga SC, amesema amepata taarifa za Hamisi Kiiza kufiwa na baba yake na pamoja na kumpa ‘pole’ wamemruhusu kurejea Uganda kwenye msiba.
Baada ya Uganda kutolewa na Tanzania Bara katika Robo Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge, Kiiza alitakiwa kwenda Dar es Salaam kuungana na wenzake walio mazoezini kujiandaa na mchezo dhidi ya Simba wa Nani Mtani Jembe, wiki mbili zijazo.
Lakini kutokana na kufiwa na baba yake, mdogo mjini Kampala, Katabaro aliyekuwa Mombasa wakati Bara inaitoa Uganda, alisema; “Kiiza ametoa taarifa za msiba na tumemruhusu kurejea Uganda, akimaliza msiba atakuja Dar es Salaam,”alisema.
MUSSA Katabaro, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu ya Yanga SC, amesema amepata taarifa za Hamisi Kiiza kufiwa na baba yake na pamoja na kumpa ‘pole’ wamemruhusu kurejea Uganda kwenye msiba.
![]() |
| Hamisi Kiiza kulia anarejea Uganda kwenye msiba, kabla ya kujiunga na Yanga kwa maandalizi ya pambano na Simba SC |
Baada ya Uganda kutolewa na Tanzania Bara katika Robo Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge, Kiiza alitakiwa kwenda Dar es Salaam kuungana na wenzake walio mazoezini kujiandaa na mchezo dhidi ya Simba wa Nani Mtani Jembe, wiki mbili zijazo.
Lakini kutokana na kufiwa na baba yake, mdogo mjini Kampala, Katabaro aliyekuwa Mombasa wakati Bara inaitoa Uganda, alisema; “Kiiza ametoa taarifa za msiba na tumemruhusu kurejea Uganda, akimaliza msiba atakuja Dar es Salaam,”alisema.
![]() |
| Katabaro wa pili kushoto akiwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Geoffrey Nyange 'Kaburu' kulia kwake |




.png)
0 comments:
Post a Comment