• HABARI MPYA

    Saturday, December 07, 2013

    STARS...ILIVYOKUWA RAHA LEO MOMBASA WAKIMVUA UBINGWA UGANDA CHALLENGE

    Wachezaji wa Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars kutoka kulia, Michael Aidan, Athumani Iddi 'Chuji', Thomas Ulimwengu na Frank Domayo wakikimbia kumfuata kipa Ivo Mapunda baada ya kucheza penalti ya mshambuliaji wa Uganda, Dani Sserunkuma na kuipa Stars ushindi wa penalti 3-2, kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90, Uwanja wa Manispaa, Mombasa, Kenya hivyo kutinga Nusu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge.  

    Godfrey Kizito wa Uganda kulia akipambana na Thomas Ulimwengu wa Stars

    Ivo Mapunda akicheza penalti ya Dani Sserunkuma

    Mrisho Ngassa akitafuta mbinu za kumtoka Godfrey Kizito 

    Salum Abubakar 'Sure Boy' akimtoka Hamisi Kiiza wa Uganda

    Mbwana Samatta akimlamba chenga Nico Wadada wa Uganda

    Nahodha wa Stars, Kevin Yondan akiwapa ishara mashabiki baada ya kufunga penalti ya mwisho

    Martin Mpouga wa Uganda, akimdhibiti Thomas Ulimwengu wa Stars

    Mrisho Ngassa akitafuta njia za kuwatoka mabeki wa Uganda

    Thomas Ulimwengu wa Stars akimgeuza Kasaga Richard wa Uganda

    Wakosa penalti; Mbwana Samatta kulia na Erato Nyoni kushoto wakisikitika baada ya kukosa penalti 

    Godfrey Walusimbi akimziba Mrisho Ngassa ili mpira utoke nje

    Unawabeba sana Waganda; Mrisho Ngassa akilalamika jambo kwea refaWish Yabarow kutoka Somalia, huku Emmanuel Okwi wa Uganda akimuangalia

    Salum Abubakar 'Sure Boy' wa Stars akigombea mpira na Emmanuel Okwi wa Uganda kushoto

    Mbwana Samatta akiwatoka mabeki wa Uganda

    Mbwana Samatta akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Uganda, 

    Samatta akitafuta njia za kumtoka beki wa Uganda Godfrey Kizito 

    Kikosi cha Stars leo

    Kikosi cha Uganda

    Shabiki maarufu wa Tanzania, Ally akiishangilia Stars leo Mombasa

    Moja kwa moja hadi Kampala; Kocha wa Uganda, Mserbia, Milutin Sredojevic 'Micho' kulia akiondoka uwanjani baada ya mechi. Uganda inarejea Uganda baada ya kutolewa na Stars leo

    Mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Malota Soma 'Ball Juggler' alikuwepo uwanjani leo kuisapoti Stars 

    Mshambuliaji wa zamani wa Yanga SC, Iddi Moshi 'Nyamwezi' alikuwepo pia tena na vazi la kizalendo kabisa
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: STARS...ILIVYOKUWA RAHA LEO MOMBASA WAKIMVUA UBINGWA UGANDA CHALLENGE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top