• HABARI MPYA

    Sunday, March 04, 2012

    YANGA YAFA KIUME CAIRO

    WAWAKILISHI wa Tanzania Bara kwenye Ligi ya Mabingwa Yanga jana waliaga michuano hiyo baada ya kufungwa bao 1-0 na Zamalek katika mechi iliyochezwa Cairo.
    Katika mechi hiyo Yanga ilicheza pungufu kuanzia dakika ya 63 baada ya mchezaji wake Athumani Iddi ‘Chuji’ kutolewa kwa kadi nyekundu kutokana na mchezo mbaya.

    Bao la Zamalek lilifungwa dakika ya 31 kupitia kwa mchezaji wake Ahmed Hossan ‘Mido’, dakika ya 78 Zamalek walipata penati lakini walikosa baada ya mpira kugonga mwamba.

    Kwa matokeo hayo, Yanga sasa imeaga michuano kwa kufungwa mabao 2-1. mechi ya

    kwanza timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1 Dar es Salaam.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA YAFA KIUME CAIRO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top