HALI ya Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji Jumatano iliyopita kwenye Hospitali ya Apollo nchini India.
Akizungumza jijini jana Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema Osiah anaendelea vizuri na atakuwa kwenye chumba maalumu kwa muda wa siku sita na baadaye kuhamishiwa kwenye wodi kwa muda wa siku 16.
Wambura alifafanua kuwa kwa ujumla matibabu yake yatachukua muda wa mwezi mmoja.
Katibu Mkuu huyo aliondoka nchini Februari 23 kuelekea nchini India kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa kichwa baada ya kubainika kuwa alikuwa na uvimbe.
Akizungumza jijini jana Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema Osiah anaendelea vizuri na atakuwa kwenye chumba maalumu kwa muda wa siku sita na baadaye kuhamishiwa kwenye wodi kwa muda wa siku 16.
Wambura alifafanua kuwa kwa ujumla matibabu yake yatachukua muda wa mwezi mmoja.
Katibu Mkuu huyo aliondoka nchini Februari 23 kuelekea nchini India kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa kichwa baada ya kubainika kuwa alikuwa na uvimbe.



.png)
0 comments:
Post a Comment