• HABARI MPYA

    Monday, January 01, 2024

    ARSENAL WALIVYOUAGA VIBAYA MWAKA 2023


    JANA Arsenal waliuaga mwaka 2023 kwa majonzi baada ya kuchapwa mabao 2-1 na wenyeji Fulham katika mchezo wa kufungia mwaka wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Craven Cottage Jijini London.
    Arsenal walitangulia kwa bao la Bukayo Saka dakika ya tano, kabla ya Fulham kutoka nyuma kwa mabao ya Raul Jimenez dakika ya 29 na Bobby Decordova-Reid dakika ya 59.
    Kwa ushindi huo, Fulham wamefikisha pointi 24 na kusogea nafasi ya 13, wakati Arsenal baada ya kipigo hicho cha pili mfululizo wanabaki na pointi zao 40 katika nafasi ya nne kufuatia timu zote kucheza mechi 20.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL WALIVYOUAGA VIBAYA MWAKA 2023 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top