KLABU ya Simba imemsajili mshambuliaji wa Kimataifa wa Gambia, Pa Omar Jobe (25) kutoka Zhenis ya Kazakhstani, huyo akiwa mchezaji wa nne mpya dirisha hili dogo.
Wapya wengine Simba SC ni mshambuliaji Saleh Karabaka Kikuya (23) kutoka JKU na viungo Msenegal, Babacar Sarr (26) kutoka US Monastir ya Tunisia na winga, Ladaki Juma Chasambi (19) kutoka Mtibwa Sugar.
0 comments:
Post a Comment