• HABARI MPYA

    Tuesday, January 30, 2024

    MZIZE APIGA TATU YANGA YASHINDA 5-1 ASFC


    KIKOSI cha Yanga leo kimefanikiwa kutinga Raundi ya Tatu ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federatión Cup (ASFC) kufuatia ushindi wa 5-1 dhidi ya Hausung ya Njombe Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
    Mabao ya Yanga leo yamefungwa na kiungo, Jonás Mkude dakika ya 20, winga Mahalatse ‘Skudu’ Makudubela dakika ya 25 na mshambuliaji Clement Mzize, matatu dakika za 27,33 na 57, wakati bao pekee la Hausung limefungwa na Tonny Jailos dakika ya 70.
    Mechi nyingine za Azam Sports Federatión Cup leo Mtibwa Sugar imeichapa Nyakagwe mabao 3-0 Uwanja wa Manungu Complex, Turiani mkoani Morogoro na Kagera Sugar imeilaza Dar City 4-0 Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
    Raundi ya Pili ya ASFC itakamilishwa kesho kwa mchezo kati ya Simba SC na Tembo FC ya Tabora Uwanja wa Azam Complex.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MZIZE APIGA TATU YANGA YASHINDA 5-1 ASFC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top