TIMU ya Manchester United imepata ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Leicester City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa King Power, Leicester, Leicestershire.
Bao pekee la Man United jana limefungwa na Jadon Sancho dakika ya 23 akimalizia pasi ya Muingereza mwenzake, Marcus Rashford.
Huo unakuwa ushindi wa tatu mfululizo chini ya kocha mpya, Mholanzi Erik ten Hag baada ya mwanzo mbaya wakipoteza mechi mbili mfululizo.
0 comments:
Post a Comment