TIMU ya Manchester City imepata ushindi mnono ugenini wa 4-0 dhidi ya wenyeji, Sevilla katika mchezo wa Kundi G Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa Ramón Sánchez Pizjuán Jijini Sevilla.
Mabao ya Man City katika mchezo huo wa kwanza Hatua ya makundi yalifungwa na mshambuliaji mpya, Mnorway Erling Haaland mawili dakika ya 20 na 67, Phil Foden dakika ya 58 na Ruben Dias dakika ya 90.
0 comments:
Post a Comment