Nahodha wa Leicester City, Wes Morgan (kushoto) akikimbia kushangilia baada ya kufunga bao la kwanza dakika ya 27 katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Sevilla kwenye mchezo wa marudiano wa 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana Uwanja wa King Power mjini Leicester, Leicestershire, England. Bao la kwanza llilifungwa na Marc Albrighton dakika ya 54 katika mchezo ambao Sevilla ilimaliza pungufu baada ya Samir Nasri kuonyeshwa kadi ya pili ya njano na kutolewa kwa kadi nyekundu kufuatia kumchezea rafu Jamie Vardy na Leicester inakwenda Robo Fainali kwa ushindi wa jumla wa 3-2, baada ya kufungwa 2-1 kwenye mchezo wa kwanza Hispania PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Ministers warn petrol retailers against ‘unfair practices’
-
Chancellor Rachel Reeves and Energy Secretary Ed Miliband called in
forecourt operators in response to the Middle East crisis.
23 minutes ago



.png)
0 comments:
Post a Comment