SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limekiri kupokea barua ya kampuni ya GSM kujitoa katika orodha ya wadhamini wa Ligi Kuu, lakini imesema itaifanyia kazi aria hiyo kabla ya kutoa majibu.
Jioni ya leo GSM imetangaza kujitoa katika orodha ya wadhamini wa Ligi Kuu kwa kile ilichokieleza TFF na Bodi ya Ligi (TPLB) kushindwa kutekeleza makubaliano.
Aidha, Mwenyekiti wa kampuni hiyo, Gharib Said Mohamed amejiuzulu Uenyekiti wa Kamati ya Taifa Stars kuanzia leo.
0 comments:
Post a Comment