MABAO ya washambuliaji, Mzambia Rodgers Kola na Mzimbabwe, Prince Dube yameipa Azam FC ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji, Pamba FC katika mchezo wa kirafiki jioni ya leo Uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza.
Azam FC imewasili Mwanza jana kuweka kambi fupi kujiandaa na mchezo wake ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya wenyeji, Biashara United Februari 22 Uwanja wa Karume mjini Musoma mkoani Mara.
0 comments:
Post a Comment