• HABARI MPYA

    Thursday, February 17, 2022

    AZAM FC YAICHAPA PAMBA FC 2-0 MECHI YA KIRAFIKI


    MABAO ya washambuliaji, Mzambia Rodgers Kola na Mzimbabwe, Prince Dube yameipa Azam FC ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji, Pamba FC katika mchezo wa kirafiki jioni ya leo Uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza. 
    Azam FC imewasili Mwanza jana kuweka kambi fupi kujiandaa na mchezo wake ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya wenyeji, Biashara United Februari 22 Uwanja wa Karume mjini Musoma mkoani Mara.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC YAICHAPA PAMBA FC 2-0 MECHI YA KIRAFIKI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top