KLABU ya Tanzania Prisons imeamua kurejesha mechi zake za nyumbani Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya kuanzia hatua iliyobaki ya msimu.
Hatua hiyo inafuatia mwenendo mbaya katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa msimu wa pili mfululizo sasa tangu ihamie Uwanja wa Nelson Mandela, Sumbawanga mkoani Rukwa.
Kwa sasa Tanzania Prisons inashika mkia katika Ligi Kuu, ikiwa imeambulia pointi 11 tu katika mechi 14.
0 comments:
Post a Comment