• HABARI MPYA

    Sunday, February 20, 2022

    SIMBA SC YALAZIMISHA SARE YA 1-1 GENDARMERIE NIAMEY


    MABINGWA wa Tanzania, Simba SC wamelazimisha sare ya 1-1 na wenyeji, Union Sportive Gendarmerie Nationale usiku wa leo Uwanja wa wa Jénérali Seyni Kountché Jijini Niamey nchini Niger katika mchezo wa Kundi D Kombe la Shirikisho Afrika.
    Wenyeji, Gendarmerie walitangulia kwa bao la Wilfried Gbeuli dakika ya 12, kabla ya winga Mghana, Bernard Morrison kuisawazishia Simba dakika ya 84.
    Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi nne na kupanda kileleni wakifuatiwa na RS Berkane ya Morocco yenye pointi tatu sawa na ASEC Mimosa ya Ivory Coast, wakati Gendarmerie Leeds inakamilisha mechi mbili bila pointi za inaendelea kushika mkia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC YALAZIMISHA SARE YA 1-1 GENDARMERIE NIAMEY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top