• HABARI MPYA

    Monday, February 28, 2022

    FIFA YAIZUIA URUSI KICHEZA NYUMBANI NA...


    SHIRIKISHO la Soka la Kimataifa (FIFA) limeitaka Urusi kucheza michezo yake katika Uwanja huru na bila mashabiki ikiwa ni kikwazo baada ya majeshi ya nchi hiyo kuivamia Ukraine na kuishambulia.
    Hata hivyo, FIFA imesema timu za Urusi zitashiriki mashindano yote ya bodi hiyo ya soka duniani, ikiwemo Kombe la Dunia baadaye mwaka huu nchini Qatar.
    Lakini FIFA imesema katika michezo ya Urusi hakutapeperushwa bendera ya nchi yao wala kuchezwa wimbo wa taifa lao.
    FIFA imesema agizo hilo litaanza kwenye michezo ya mchujo wa kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Poland Machi ambao ulipangwa kuchezwa Jijini Moscow.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FIFA YAIZUIA URUSI KICHEZA NYUMBANI NA... Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top