• HABARI MPYA

    Wednesday, February 16, 2022

    SIMBA SC YATINGA ROBO FAINALI ASFC KIBABE HASWA


    MABINGWA watetezi, Simba SC wametinga Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) kwa kishindo baada ya ushindi wa 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
    Mabao ya Simba SC yamefungwa na Nahodha, John Bocco mawili dakika ya pili n 40, Clatous Chama matatu dakika ya 23, 25 na 73, Masinda aliyejifunga dakika ya 44 na Jimson Mwanuke dakika ya 70.
    Timu nyingine zilizofuzu Robo Fainali ni Azam FC iliyoichapa Baga Friends 6-0, Geita Gold iliyoichapa Mbuni FC 1-0, Coastal Union iliyoichapa Mtibwa Sugar 2-0, Kagera Sugar iliyoilaza Namungo FC 1-0, Polisi Tanzania iliyoipiga Tanzania Prisons 2-0, Yanga SC iliyolaza Biashara United 2-1 na timu pekee isiyo ya Ligi Kuu, Pamba ambayo imeitoa Dodoma Jiji FC.
    Droo ya Robo Fainali itafuatia wiki ijayo na mechi za hatua hiyo ya Nane Bora zitachezwa mwezi ujao.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    1 comments:

    Unknown said... March 25, 2022 at 1:16 AM

    The Best Slots | Casino Roll
    The best slots at Casino Roll. If you gri-go.com love table 카지노 games, to play blackjack, you have 우리 카지노 본사 to bet twice for the dealer to 사이트 추천 win. The dealer bet 365 must

    Item Reviewed: SIMBA SC YATINGA ROBO FAINALI ASFC KIBABE HASWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top