MLINDA mlango wa kimataifa wa Mali, Djigui Diarra akiwa mazoezini na klabu yake, Yanga SC baada ya kurejea nchini kutoka nchini Cameroon alipokuwa na timu yake ya taifa kwa ajili ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zilizomalizika Jumapili kwa Senegal kuwa mabingwa.
Baada ya kukosekana tangu mwishoni mwa Desemba, Diarra anatarajiwa kuonekana tena kazini Yanga ikimenyana na Biashara United katika mchezo wa Hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) Jumanne Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment