• HABARI MPYA

    Sunday, February 20, 2022

    LIVERPOOL YAICHAPA NORWICH CITY 3-1 ANFIELD


    WENYJI, Liverpool jana waliitandika Norwich City mabao 3-1 Uwanja wa Anfield katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
    Milot Rashica alianza kuifungia Norwich dakika ya 48, kabla ya Liverpool kutoka nyuma kwa mabao ya Sadio Mané dakika ya 64, Mohamed Salah 67 na mchezaji mpya, Luis  Díaz 81.
    Kwa ushindi huo, Liverpool inafikisha pointi 57 katika mchezo wa 25, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi sita na vinara, Manchester City ambao pia wana mechi moja mkononi.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL YAICHAPA NORWICH CITY 3-1 ANFIELD Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top