• HABARI MPYA

    Tuesday, February 22, 2022

    BIASHARA UNITED YAICHAPA AZAM FC 2-0 KIRUMBA


    MABAO ya Collins Opare dakika ya  49 na James Shagara dakika ya 90 na ushei yameipa Biashara United ushindi wa 2-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.
    Kwa ushindi huo, Biashara inafikisha pointi 15 na kumaliza mechi 15 za mzunguko wa kwanza katika nafasi ya 12, wakati Azam FC inabaki na pointi zake 24 za mechi 15 pia katika nafasi ya tatu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BIASHARA UNITED YAICHAPA AZAM FC 2-0 KIRUMBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top