TIMU ya Manchester City imepata ushindi mwembamba wa 2-1 dhidi ya Borussia Dortmund katika mchezo wa kwanza wa Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa Etihad.
Mabao ya Manchester City yamefungwa na viungo wa kimataifa wa Ubelgiji, Kevin De Bruyne dakika ya 19 na England, Philip Foden dakika ya 90, wakati la Borussia Dortmund limefungwa na mshambuliaji Mjerumani, Marco Reus dakika ya 84 na timu hizo zitarudiana Aprili 14 Uwanja wa Signal-Iduna-Park Jijini Dortmund na wenyeji watajitaji ushindi wa 1-0 kwenda Nusu Fainali .
0 comments:
Post a Comment