LICHA ya kuchapwa 1-0 na FC Porto jana, timu ya Chelsea ya England imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa ushindi wa jumla wa 2-1 katika mchezo wa kwanza wiki ilioypita, mechi zote zikichezwa Uwanja wa Ramon Sanchez Pizjuan Jijini Sevilla, Hispania.
Bao la Porto jana lilifungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Iran, Mehdi Taremi dakika ya 90 na ushei na Chelsea sasa itakutana na mshindi wa jumla kati ya Real Madrid na Liverpool zinazomenyana leo Uwanja Anfield. Real ilishinda 3-1 mechi ya kwanza nyumbani.
0 comments:
Post a Comment