KLABU ya Yanga SC leo imemtambulisha rasmi Mtunisia, Mohamed Nasreddine Nabi kuwa kocha wake mpya Mkuu, akichukua nafasi ya Mrundi, Cedric Kaze aliyefukuzwa mwezi uliopita.
Pamoja na Nabi, Yanga imemtambulisha
Mtunisia mwenzake, Sghir Hammadi kuwa Kocha Msaidizi, wote wawili wakisaini mkataba wa mwaka mmoja na nusu.
"Nina furaha sana kuwa hapa, Yanga ni timu kubwa na nina matarajio makubwa ndani ya timu hii” amesema Nabi.
0 comments:
Post a Comment