TIMU ya Chelsea imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la FA England baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Manchester City katika mchezo wa Nusu Fainali leo Uwanja wa Wembley Jijini London.
Bao pekee la The Blues leo limefungwa na kiungo Mmorocco mzaliwa wa Uholanzi, Hakim Ziyech dakika ya 55 akimalizia pasi ya mshambuliaji Mjerumani, Timo Werner na sasa itakutana na mshindi kati ya Leicester City na Southampton zinazomenyana kesho.
0 comments:
Post a Comment