• HABARI MPYA

    Wednesday, December 21, 2016

    KAHEMELE, KAWEMBA, BARAKA 'WATEMWA', ILA...

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    VIONGOZI wa klabu za Azam, Simba na Yanga waliokamatwa kwa makosa tofauti ya kuajiri na kuwatumikisha wageni bila kuwa na vibali vya Idara ya Uhamiaji kwa mujibu wa sheria wamechiwa.
    Habari za ndani ambazo Bin Zubeiry Sports – Online imezipata zinasema kwamba Mtendaji Mkuu wa Azam, Saad Kawemba na Makatibu Wakuu wa Simba, Patrick Kahemele na Yanga Baraka Deusdedit wamechiwa baada ya kuhojiwa kwa saa kadhaa.
    Kwa pamoja wote walikamatwa kwa tuhuma za kuwaruhusu wachezaji na makocha wao wa kigeni kufanya kazi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara mwishoni mwa wiki bila na vibali.
    Patrick Kahemele (kushoto) leo 'amekula kibano' cha makamanda wa Uhamiaji hadi kijasho chembamba kikamtoka 

    Yanga iliifunga JKT Ruvu 3-0 Jumamosi na Jumapili Azam ikalazimishwa sare ya 0-0 na African Lyon mechi zote zikipigwa Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam huku Simba ikishinda 2-0 dhidi ya Ndanda FC Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.
    Upande wa Azam wanaodaiwa kucheza bila kuwa na vibali ni beki Yakubu Mohammed, washambuliaji Yahaya Mohammed, Samuel Afful wote kutoka Ghana na kiungo mkabaji Stephan Kingue Mpondo kutoka Cameroon.
    Kwa Simba wanaodaiwa kucheza bila kuwa na vibali ni kipa Daniel Agyei na kiungo James Kotei, wakati Yanga inatuhumiwa kuwatumia makocha wake, George Lwandamina na Noel Mwandila wakiwa hawana vibali.
    Kiungo mpya wa Yanga, Justin Zulu hakucheza mwishoni mwa wiki na alikuwa jukwaani.
    Na baada ya kuhojiwa kwa saa kadhaa kufuatia kukamatwa asubuhi, viongozi hao wakaachiwa kwa masharti ya kutorudia makosa ya aina hiyo. Na wameambiwa wahakikishe wachezaji wote wanakamilisha taratibu za Uhamiaji haraka iwezekanavyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAHEMELE, KAWEMBA, BARAKA 'WATEMWA', ILA... Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top