• HABARI MPYA

    Friday, April 17, 2015

    WIKI MBILI KABLA YA KUKUTANA ULINGONI, MAYWEATHER NA PACQUIAO WATAMBIANA KWA STAHILI HII...

    ZIKIWA zimebaki wiki mbili kabla ya pambano lao la dola za Kimarekani Milioni 300, mabondia Floyd Mayweather na Manny Pacquiao wameonyesha jinsi walivyo fiti miili yao wakati wakiendelea na maandalizi.
    Pambano hilo litafanyika mjini Las Vegas, katika ukumbi wa MGM Grand Garden Arena Mei 2 - likipewa hadhi ya pambano kubwa zaidi katika historia ya ndondi duniani. 
    Na bondia huyo wa Ufilipino amekuwa akionyesha namna alivyo fiti akiposti picha kuonyesha mwili wake uliojengeka kimichezo wiki za karibuni.
    Manny Pacquiao used Instagram to show his fans a photo of his ripped body as he continues his preparation
    Manny Pacquiao ametumia Instagram kuwaonyesha mashabiki wake mwili wake ulivyo wakati akiendelea na maandalizi
    The Filipino fighter is looking to put an end to Floyd Mayweather's current unbeaten record in the ring
    Bondia huyo wa Ufilipino anatazamiwa kuvunja rekodi ya Floyd Mayweather kutopigwa hadi sasa katika ngumi za kulipwa

    Katika posti yake ya siku za karibuni kwenye Instagram, amesema: 'Zimebaki siku 16. Niko tayari kuingia. #MayPac.' 
    Mayweather naye aameendelea na kampeni yake ya promo, baada ya bingwa huyo wa dunia ambaye hajapoteza pambano kuweka rekodi yake ya kushinda mapambano yote 47. 
    Msanii wa muziki, Liljamez ameposti picha ya 'Money' Mayweather, ambaye anatarajiwa kulipwa Pauni Milioni 180 kwenye pambano hilo. Music artist Liljamez posted the photo of 'Money' with just over two weeks to go until the $300million fight

    Msanii wa muziki, Liljamez ameposti picha hii ya 'Money' zikiwa zimesalia wiki mbili kuelekea pambano la dola za Kimarekani Milioni 300
    Earning an estimated $180million from the bout, Mayweather is confident he won't lose his perfect record
    Mayweather amekuwa pia akiposti picha za namna anavyojifua
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WIKI MBILI KABLA YA KUKUTANA ULINGONI, MAYWEATHER NA PACQUIAO WATAMBIANA KWA STAHILI HII... Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top